Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yeremia 28
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Yeremia—Yaliyomo

      • Nabii wa uwongo Hanania ampinga nabii Yeremia (1-17)

Yeremia 28:1

Marejeo

  • +2Fa 24:17; 2Nya 36:10
  • +Yos 11:19; 2Sa 21:2

Yeremia 28:2

Marejeo

  • +Yer 27:4, 8

Yeremia 28:3

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “miaka miwili ya siku.”

Marejeo

  • +2Fa 24:11, 13; Yer 27:16; Da 1:2

Yeremia 28:4

Marejeo

  • +2Fa 24:8; 25:27; Yer 37:1
  • +2Fa 23:36; 24:6
  • +2Fa 24:12, 14; Yer 24:1

Yeremia 28:6

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “Na iwe hivyo!”

Yeremia 28:10

Marejeo

  • +Yer 27:2

Yeremia 28:11

Marejeo

  • +Yer 28:4

Yeremia 28:13

Marejeo

  • +Yer 27:2

Yeremia 28:14

Marejeo

  • +Kum 28:48; Yer 5:19
  • +Yer 27:6; Da 2:37, 38

Yeremia 28:15

Marejeo

  • +Yer 28:1
  • +Yer 14:14; 23:21; 27:15; Eze 13:3

Yeremia 28:16

Marejeo

  • +Kum 13:5; 18:20; Yer 29:32

Jumla

Yer. 28:12Fa 24:17; 2Nya 36:10
Yer. 28:1Yos 11:19; 2Sa 21:2
Yer. 28:2Yer 27:4, 8
Yer. 28:32Fa 24:11, 13; Yer 27:16; Da 1:2
Yer. 28:42Fa 24:8; 25:27; Yer 37:1
Yer. 28:42Fa 23:36; 24:6
Yer. 28:42Fa 24:12, 14; Yer 24:1
Yer. 28:10Yer 27:2
Yer. 28:11Yer 28:4
Yer. 28:13Yer 27:2
Yer. 28:14Kum 28:48; Yer 5:19
Yer. 28:14Yer 27:6; Da 2:37, 38
Yer. 28:15Yer 28:1
Yer. 28:15Yer 14:14; 23:21; 27:15; Eze 13:3
Yer. 28:16Kum 13:5; 18:20; Yer 29:32
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Yeremia 28:1-17

Yeremia

28 Mwaka huohuo, mwanzoni mwa utawala wa Mfalme Sedekia+ wa Yuda, katika mwaka wa nne, mwezi wa tano, nabii Hanania mwana wa Azuri kutoka Gibeoni+ aliniambia hivi katika nyumba ya Yehova mbele ya makuhani na watu wote: 2 “Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi, ‘Nitaivunja nira ya mfalme wa Babiloni.+ 3 Katika muda wa miaka miwili* nitavirudisha mahali hapa vyombo vyote vya nyumba ya Yehova ambavyo Mfalme Nebukadneza wa Babiloni alivichukua mahali hapa na kuvipeleka Babiloni.’”+ 4 “‘Nami nitamrudisha mahali hapa Yekonia+ mwana wa Yehoyakimu,+ mfalme wa Yuda, na watu wote wa Yuda waliohamishwa na kupelekwa Babiloni,’+ asema Yehova, ‘kwa maana nitaivunja nira ya mfalme wa Babiloni.’”

5 Kisha nabii Yeremia akazungumza na nabii Hanania mbele ya makuhani na watu wote waliokuwa wamesimama katika nyumba ya Yehova. 6 Nabii Yeremia akasema: “Amina!* Yehova na afanye hivyo! Yehova na atimize maneno yako uliyotabiri kwa kuvirudisha mahali hapa vyombo vya nyumba ya Yehova kutoka Babiloni na pia watu wote waliopelekwa uhamishoni! 7 Hata hivyo, tafadhali sikia ujumbe huu ninaosema masikioni mwako na masikioni mwa watu wote. 8 Zamani za kale manabii walionitangulia mimi na waliokutangulia wewe walikuwa wakitabiri kuhusu nchi nyingi na falme kubwa, kuhusu vita, misiba, na magonjwa hatari. 9 Nabii akitabiri amani na neno la nabii huyo litimie, basi itajulikana kwamba kwa kweli Yehova amemtuma nabii huyo.”

10 Ndipo nabii Hanania akaichukua ile nira kutoka shingoni mwa nabii Yeremia na kuivunja.+ 11 Kisha Hanania akasema mbele ya watu wote: “Yehova anasema hivi: ‘Hivyo ndivyo nitakavyoivunja nira ya Mfalme Nebukadneza wa Babiloni kutoka shingoni mwa mataifa yote katika muda wa miaka miwili.’”+ Kisha nabii Yeremia akaenda zake.

12 Baada ya nabii Hanania kuivunja ile nira kutoka shingoni mwa nabii Yeremia, ujumbe huu wa Yehova ukamjia Yeremia: 13 “Nenda umwambie Hanania, ‘Yehova anasema hivi: “Umevunja nira za mbao,+ lakini badala yake utatengeneza nira za chuma.” 14 Kwa maana Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: “Nitaweka nira ya chuma juu ya shingo ya mataifa haya yote, ili yamtumikie Mfalme Nebukadneza wa Babiloni, nayo lazima yamtumikie.+ Nitampa hata wanyama wa mwituni.”’”+

15 Kisha nabii Yeremia akamwambia nabii Hanania:+ “Tafadhali, sikiliza, ewe Hanania! Yehova hakukutuma wewe, bali umewafanya watu hawa wautumaini uwongo.+ 16 Kwa hiyo Yehova anasema hivi: ‘Tazama! Ninakuondoa katika uso wa nchi. Utakufa mwaka huu, kwa maana umewachochea watu wamwasi Yehova.’”+

17 Basi nabii Hanania akafa mwaka huo, katika mwezi wa saba.

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki