9 Kisha akasema: “Ikiwa, sasa, nimepata kibali machoni pako, Ee Yehova, tafadhali, Yehova na aende pamoja nasi katikati yetu,+ kwa sababu ni watu wenye shingo ngumu,+ nawe utusamehe kosa letu na dhambi yetu,+ nawe utuchukue tuwe mali yako.”+
20 Naye atamfanya huyo ng’ombe-dume kama alivyomfanya yule ng’ombe mwingine wa toleo la dhambi. Hivyo ndivyo atakavyomfanya; naye kuhani atafanya upatanisho+ kwa ajili yao, ndipo watasamehewa.
7 Naye kuhani atafanya upatanisho+ kwa ajili yake mbele za Yehova, naye atasamehewa lolote ambalo huenda akafanya kati ya mambo yote hayo, nalo limfanye awe na hatia.”
22 Naye kuhani atafanya upatanisho kwa ajili yake kwa yule kondoo-dume wa toleo la hatia mbele za Yehova kwa ajili ya dhambi yake ambayo alitenda; naye atasamehewa dhambi yake ambayo alitenda.+