35 Na mkuu wa nyumba ya ukoo wa upande wa baba kwa ajili ya familia za Merari alikuwa Zurieli mwana wa Abihaili. Walipiga kambi upande wa maskani kuelekea kaskazini.+
38 Na wale wanaopiga kambi mbele ya maskani kuelekea mashariki, mbele ya hema la mkutano kuelekea mapambazuko ya jua, walikuwa Musa na Haruni na wanawe, wale waliokuwa wakitimiza wajibu wa patakatifu,+ kama wajibu wa wana wa Israeli. Na mgeni yeyote ambaye angekaribia angeuawa.+