Hesabu
2 Sasa Yehova akasema na Musa na Haruni, na kuwaambia: 2 “Wana wa Israeli watapiga kambi, kila mtu kulingana na mgawanyo wake wa makabila matatu,+ kando ya alama za nyumba ya baba zao. Watapiga kambi kuzunguka pande zote mbele ya hema la mkutano.
3 “Na wale wanaopiga kambi upande wa mashariki kuelekea mapambazuko ya jua watakuwa mgawanyo wa makabila matatu ya kambi ya Yuda kwa majeshi yao, na mkuu wa wana wa Yuda ni Nashoni+ mwana wa Aminadabu. 4 Na jeshi lake na wale walioandikishwa kati yao ni 74,600.+ 5 Na wale wanaopiga kambi kando yake watakuwa kabila la Isakari,+ na mkuu wa wana wa Isakari ni Nethaneli+ mwana wa Zuari. 6 Na jeshi lake na watu wake walioandikishwa ni 54,400.+ 7 Na kabila la Zabuloni; na mkuu wa wana wa Zabuloni ni Eliabu+ mwana wa Heloni. 8 Na jeshi lake na watu wake walioandikishwa ni 57,400.+
9 “Watu wote walioandikishwa wa kambi ya Yuda ni 186,400 kwa majeshi yao. Wanapaswa kuondoka kwanza.+
10 “Ule mgawanyo wa makabila matatu wa Rubeni+ utakuwa kuelekea kusini kwa majeshi yao, na mkuu wa wana wa Rubeni ni Elisuri+ mwana wa Shedeuri. 11 Na jeshi lake na watu wake walioandikishwa ni 46,500.+ 12 Na wale wanaopiga kambi kando yake watakuwa kabila la Simeoni, na mkuu wa wana wa Simeoni ni Shelumieli+ mwana wa Zurishadai. 13 Na jeshi lake na watu walioandikishwa kati yao ni 59,300.+ 14 Na kabila la Gadi; na mkuu wa wana wa Gadi ni Eliasafu+ mwana wa Reueli. 15 Na jeshi lake na watu walioandikishwa kati yao ni 45,650.+
16 “Watu wote walioandikishwa wa kambi ya Rubeni ni 151,450 kwa majeshi yao, nao wanapaswa kuondoka wakiwa wa pili.+
17 “Hema la mkutano+ litakapoondoka, kambi ya Walawi+ itakuwa katikati ya kambi hizo.
“Kama vile watakavyopiga kambi, ndivyo watakavyoondoka,+ kila mmoja mahali pake, kulingana na mgawanyo wao wa makabila matatu.
18 “Mgawanyo wa makabila matatu wa kambi ya Efraimu+ kwa majeshi yao utakuwa kuelekea magharibi, na mkuu wa wana wa Efraimu ni Elishama+ mwana wa Amihudi. 19 Na jeshi lake na watu walioandikishwa kati yao ni 40,500.+ 20 Na kando yake kutakuwa na kabila la Manase,+ na mkuu wa wana wa Manase ni Gamalieli+ mwana wa Pedazuri. 21 Na jeshi lake na watu walioandikishwa kati yao ni 32,200.+ 22 Na kabila la Benyamini;+ na mkuu wa wana wa Benyamini ni Abidani+ mwana wa Gidioni. 23 Na jeshi lake na watu walioandikishwa kati yao ni 35,400.+
24 “Watu wote walioandikishwa wa kambi ya Efraimu ni 108,100 kwa majeshi yao, nao wanapaswa kuondoka wakiwa wa tatu.+
25 “Mgawanyo wa makabila matatu wa kambi ya Dani utakuwa kuelekea kaskazini kwa majeshi yao, na mkuu wa wana wa Dani ni Ahiezeri+ mwana wa Amishadai. 26 Na jeshi lake na watu walioandikishwa kati yao ni 62,700.+ 27 Na wale wanaopiga kambi kando yake ni kabila la Asheri, na mkuu wa wana wa Asheri ni Pagieli+ mwana wa Okrani. 28 Na jeshi lake na watu walioandikishwa kati yao ni 41,500.+ 29 Na kabila la Naftali;+ na mkuu wa wana wa Naftali ni Ahira+ mwana wa Enani. 30 Na jeshi lake na watu walioandikishwa kati yao ni 53,400.+
31 “Watu wote walioandikishwa wa kambi ya Dani ni 157,600. Wanapaswa kuondoka wakiwa wa mwisho+—kulingana na mgawanyo wao wa makabila matatu.”
32 Hao ndio watu walioandikishwa wa wana wa Israeli kulingana na nyumba ya baba zao; wote walioandikishwa wa kambi hizo kwa majeshi yao walikuwa 603,550.+ 33 Lakini Walawi hawakuandikishwa+ katikati ya wana wa Israeli, kama vile Yehova alivyokuwa amemwamuru Musa. 34 Na wana wa Israeli wakafanya kulingana na yote ambayo Yehova alikuwa amemwamuru Musa.+ Hivyo ndivyo walivyopiga kambi kwa migawanyo yao ya makabila matatu,+ na hivyo ndivyo walivyoondoka,+ kila mmoja kwa familia zake kulingana na nyumba ya baba zake.