24 Kwa maana nitayafukuzia mbali mataifa toka mbele yako,+ nami nitalipanua eneo lako;+ wala hakuna mtu yeyote atakayeitamani nchi yako wakati utakapokuwa ukienda kuuona uso wa Yehova Mungu wako mara tatu kwa mwaka.+
8 “‘Mwishowe nikawaleta ninyi katika nchi ya Waamori waliokuwa wakikaa ng’ambo ile nyingine ya Yordani, nao wakaanza kupigana nanyi.+ Ndipo nikawatia mkononi mwenu ili kuimiliki nchi yao, nami nikawaangamiza kutoka mbele yenu.+