21 Na Mfalme Yehoyakimu+ na wanaume wake wote wenye nguvu na wakuu wote wakayasikia maneno yake, na mfalme akaanza kutafuta kumuua.+ Uriya aliposikia habari hizo, akaogopa+ mara moja, akakimbia, akaingia Misri.
32 Na Yeremia akachukua kitabu kingine cha kukunjwa, akampa Baruku mwana wa Neria, mwandishi,+ ambaye aliandika juu yake kutoka kinywani+ mwa Yeremia maneno yote ya kile kitabu ambacho Yehoyakimu mfalme wa Yuda alikuwa ameteketeza motoni;+ na maneno mengine mengi kama hayo yakaongezwa kwenye hayo.