7 Pia, katika siku za Artashasta, Bishlamu, Mithredathi, Tabeeli na wale wenzake walimwandikia Artashasta mfalme wa Uajemi, na maandishi ya barua hiyo yaliandikwa kwa herufi za Kiaramu na kutafsiriwa katika lugha ya Kiaramu.+
23 Ikawa kwamba baada ya kusomwa kwa nakala ya barua rasmi ya Mfalme Artashasta mbele ya Rehumu+ na Shimshai+ mwandishi na wenzao,+ walifanya haraka kwenda Yerusalemu kwa Wayahudi na kuwakomesha kwa kutumia nguvu za silaha.+
7 Basi ikawa kwamba, mara tu Sanbalati+ na Tobia+ na Waarabu+ na Waamoni+ na Waashdodi+ waliposikia kwamba kazi ya kurekebisha kuta za Yerusalemu imesonga mbele, kwa maana mashimo yalikuwa yameanza kuzibwa, wakakasirika sana.