14 Nawe utashangilia wakati wa sherehe yako,+ wewe na mwana wako na binti yako na mtumishi wako na kijakazi wako na Mlawi na mkaaji mgeni na mvulana asiye na baba na mjane, walio ndani ya malango yako.
15 Siku saba utamfanyia Yehova Mungu wako sherehe+ katika mahali ambapo Yehova atapachagua, kwa sababu Yehova Mungu wako atakubariki+ katika mazao yako yote na katika kila tendo la mkono wako, nawe utakuwa na shangwe kwelikweli.+