16 Upotovu wenu! Je, mfinyanzi ahesabiwe kama udongo?+ Kwa maana, je, kitu kilichofanywa kiseme hivi kumhusu mwenye kukifanya: “Yeye hakunifanya”?+ Na je, kitu ambacho kimefanywa kwa kweli kiseme kumhusu mwenye kukifanya: “Hakuonyesha uelewaji”?+
6 “‘Je, mimi siwezi kuwatendea kama mfinyanzi huyu alivyotenda, enyi nyumba ya Israeli?’ asema Yehova. ‘Tazama! Kama udongo mkononi mwa mfinyanzi, ndivyo ninyi mlivyo mkononi mwangu, enyi nyumba ya Israeli.+