Ayubu
10 “Nafsi yangu inahisi kuchukizwa na uhai wangu.+
Nitaonyesha hangaiko langu kujihusu mwenyewe.
Nitasema kwa uchungu wa nafsi yangu!
2 Nitamwambia Mungu, ‘Usinitangaze kuwa mwovu.
Nijulishe kwa nini unashindana nami.
3 Je, ni vema kwako kwamba wewe utende kosa,+
Kwamba ukatae tokeo la kazi yenye nguvu ya mikono yako,+
Na kwamba kwa kweli uangazie shauri la waovu?
5 Je, siku zako ni kama siku za mwanadamu anayeweza kufa,+
Au, miaka yako ni kama siku za mwanamume,
6 Kwamba ujaribu kutafuta kosa langu
Nawe uendelee kuitafuta dhambi yangu?+
8 Mikono yako mwenyewe imeniunda hivi kwamba ikanifanyiza mimi+
Mzima pande zote, na bado unataka kunimeza.
9 Tafadhali, kumbuka kwamba umenifanyiza kutoka katika udongo+
Nawe utanifanya nirudi katika mavumbi.+
13 Nawe umeficha mambo hayo moyoni mwako.
Ninajua vema kwamba una mambo hayo.
14 Ikiwa nimetenda dhambi na umeendelea kunitazama+
Nawe hunichukulii kuwa sina hatia katika kosa langu;+
15 Ikiwa kweli nimekosea, ole wangu!+
Na ikiwa kweli niko upande wa haki, nisipate kuinua kichwa changu,+
Nikiwa nimejawa sana na aibu na kujawa na mateso.+
16 Nacho kikitenda kwa majivuno,+ utaniwinda kama mwana-simba,+
Nawe utajionyesha tena kuwa wa ajabu kwangu.
17 Utaleta mashahidi wako wapya mbele yangu,
Nawe utafanya usumbufu wako kuwa mkubwa zaidi juu yangu;
Magumu baada ya magumu yako pamoja nami.
18 Basi kwa nini ulinitoa nje ya tumbo la uzazi?+
Kama ningekata pumzi, ili hata jicho lisinione,
19 Ningekuwa kana kwamba sijapata kuwako;
Ningeletwa kutoka tumboni mpaka kaburini.’
22 Kwenye nchi ya giza kama weusi, ya kivuli kizito
Na ya mchafuko, ambako hakuangazi zaidi ya weusi.”