Ayubu
11 Naye Sofari Mnaamathi+ akajibu, akasema:
2 “Je, maneno mengi yatakosa kujibiwa,
Au, je, mwenye kujisifu tu atakuwa upande wa haki?
3 Je, maongezi yako matupu yatawanyamazisha watu,
Na je, utaendelea kudharau bila kuwa na mtu wa kukukemea?+
6 Ndipo angekuambia siri za hekima,
Kwa kuwa mambo ya hekima inayotumika ni mengi.
Pia, ungejua kwamba Mungu anaruhusu sehemu ya makosa yako yasahaulike kwa ajili yako.+
7 Je, unaweza kuvumbua mambo yenye kina ya Mungu,+
Au, je, unaweza kuvumbua kikomo chenyewe cha Mweza-Yote?
8 Iko juu kuliko mbingu. Wewe unaweza kutimiza nini?
9 Ina kipimo kirefu kuliko dunia,
Na ni pana kuliko bahari.
10 Akisonga mbele na kumshika mtu
Na kuita mahakama, basi ni nani anayeweza kumpinga?
11 Kwa kuwa yeye mwenyewe anajua vema watu wasiosema kweli.+
Anapoona jambo lenye kudhuru, je, yeye pia hatalikazia uangalifu?
12 Hata mtu asiye na akili atapata kusudi jema
Mara tu punda-mwitu anapozaliwa kuwa mwanadamu.
14 Ikiwa jambo lenye kudhuru limo mkononi mwako, liondolee mbali kabisa,
Wala usiache ukosefu wa uadilifu ukae katika mahema yako.
16 Kwa maana wewe—utaisahau taabu;
Utaikumbuka kama maji ambayo yamepita.
17 Na urefu wa maisha yako+ utainuka kwa wangavu kuliko katikati ya mchana;
Giza litakuwa kama asubuhi.+
18 Nawe utakuwa na tegemeo kwa maana kuna tumaini;
Nawe utatazama huku na huku kwa uangalifu—utalala kwa usalama.+