5 “Na, tazama! mnyama mwingine, wa pili, aliye kama dubu.+ Naye alikuwa ameinuliwa upande mmoja,+ na kulikuwa na mifupa mitatu ya mbavu kinywani mwake kati ya meno yake; nao walikuwa wakimwambia hivi, ‘Simama, ule nyama nyingi.’+
3 Nilipoinua macho yangu, ndipo nikaona, na, tazama! kondoo-dume+ amesimama mbele ya huo mfereji, naye alikuwa na pembe mbili. Na hizo pembe mbili zilikuwa ndefu, lakini moja ilikuwa ndefu kuliko ile nyingine, na ile ndefu ndiyo iliyotokea baadaye.+
“Tazama! Bado kutakuwa na wafalme watatu wenye kusimama kwa ajili ya Uajemi,+ na yule wa nne+ atakusanya utajiri mwingi kuliko wengine wote.+ Na mara tu atakapopata nguvu katika utajiri wake, ataamsha kila kitu kupigana na ufalme wa Ugiriki.+