27 walikuwa wakila, walikuwa wakinywa, wanaume walikuwa wakioa, wanawake walikuwa wakiolewa, mpaka siku ile ambayo Noa aliingia katika safina, na gharika ikafika na kuwaangamiza wote.+
7 Kwa imani Noa,+ baada ya kupewa onyo la kimungu la mambo ambayo yalikuwa bado hayajaonekana,+ alionyesha woga wa kimungu na kujenga safina+ kwa ajili ya kuiokoa nyumba yake; na kupitia imani hiyo aliuhukumu ulimwengu+ kuwa wenye hatia, naye akawa mrithi wa uadilifu+ unaolingana na imani.
20 ambao wakati fulani hawakuwa watiifu+ wakati subira ya Mungu+ ilipokuwa ikingoja katika siku za Noa, safina ilipokuwa ikijengwa,+ ambayo ndani yake watu wachache, yaani, nafsi nane, walichukuliwa salama kupitia maji.+
5 naye hakujizuia kuuadhibu ulimwengu wa kale,+ bali alimlinda Noa, mhubiri wa uadilifu,+ akiwa salama pamoja na wengine saba+ alipoleta gharika+ juu ya ulimwengu wa watu wasiomwogopa Mungu;