3 Kwa maana nitamimina maji juu ya mwenye kiu,+ na vijito vinavyotiririka juu ya mahali pakavu.+ Nitaimimina roho yangu juu ya uzao wako,+ na baraka yangu juu ya wazao wako.
28 “Kisha itakuwa kwamba nitaimimina roho yangu+ juu ya kila namna ya mwili,+ na wana wenu na binti+ zenu watatoa unabii. Nao wazee wenu wataota ndoto. Nao wanaume wenu vijana wataona maono.
33 Hata sikumjua, bali Yule aliyenituma+ nibatize katika maji aliniambia, ‘Yeyote yule ambaye utaona roho ikishuka na kukaa juu yake, huyo ndiye ambaye hubatiza katika roho takatifu.’+
17 ‘ “Na katika siku za mwisho,” Mungu asema, “Nitaimimina sehemu ya roho yangu+ juu ya kila namna ya mwili, nao wana wenu na binti zenu watatoa unabii nao wanaume wenu vijana wataona maono na wazee wenu wataota ndoto;+