8 Wakamjibu: “Kila mmoja wetu aliota ndoto lakini hakuna mtu wa kutueleza maana yake.”* Yosefu akawaambia: “Je, si kazi ya Mungu kueleza maana ya ndoto?+ Tafadhali, nisimulieni ndoto zenu.”
28 Lakini kuna Mungu mbinguni ambaye ni Mfunuaji wa siri,+ naye amekujulisha wewe Mfalme Nebukadneza mambo yatakayotukia katika kipindi cha mwisho cha zile siku. Hii ndiyo ndoto yako, na haya ndiyo maono yaliyokujia kichwani ulipokuwa umelala kitandani: