-
Mwanzo 47:29-31Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
29 Wakati wa Israeli kufa ulikuwa ukikaribia,+ kwa hiyo akamwita Yosefu mwanawe na kumwambia: “Ikiwa sasa nimepata kibali machoni pako, tafadhali, weka mkono wako chini ya paja langu, na unitendee kwa upendo mshikamanifu na uaminifu. Tafadhali, usinizike Misri.+ 30 Nitakapokufa,* unapaswa kunibeba na kunitoa Misri na kunizika katika kaburi la mababu zangu.”+ Basi Yosefu akasema: “Nitafanya tu kama unavyosema.” 31 Kisha Yakobo akasema: “Niapie.” Basi akamwapia.+ Ndipo Israeli akainama upande wa kichwa cha kitanda chake.+
-