-
Mwanzo 28:16-19Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
16 Kisha Yakobo akaamka kutoka usingizini na kusema: “Kwa kweli Yehova yuko mahali hapa, nami sikujua.” 17 Naye akaogopa na kusema: “Mahali hapa panaogopesha kwelikweli! Bila shaka hapa ni nyumba ya Mungu,+ na hili ndilo lango la mbingu.”+ 18 Kwa hiyo Yakobo akaamka asubuhi na mapema na kuchukua lile jiwe alilokuwa amepumzisha kichwa chake juu yake, akalisimamisha kama nguzo na kumimina mafuta juu yake.+ 19 Basi akapaita mahali hapo Betheli,* lakini hapo awali jiji hilo liliitwa Luzi.+
-