-
2 Petro 2:6-8Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
6 Na kwa kuyageuza majiji ya Sodoma na Gomora kuwa majivu, aliyahukumu+ akiweka kielelezo kwa watu wasiomwogopa Mungu kuhusu mambo yatakayokuja.+ 7 Naye alimwokoa Loti mwadilifu,+ aliyetaabishwa sana na mwenendo mpotovu* wa waasi sheria— 8 kwa maana siku baada ya siku mtu huyo mwadilifu alikuwa akiitesa nafsi* yake yenye uadilifu kwa sababu ya matendo ya kuasi sheria aliyoona na kusikia alipokuwa akiishi miongoni mwao.
-