-
Mwanzo 21:22-24Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
22 Wakati huo Abimeleki akiwa pamoja na Fikoli mkuu wa jeshi lake akamwambia Abrahamu: “Mungu yuko pamoja nawe katika kila jambo unalofanya.+ 23 Basi sasa niapie hapa mbele za Mungu kwamba hutanitendea kwa udanganyifu mimi na watoto wangu na wazao wangu, na kwamba utanitendea kwa upendo mshikamanifu mimi na wakaaji wa nchi ambayo umekuwa ukiishi, kama nilivyokutendea kwa upendo mshikamanifu.”+ 24 Kwa hiyo Abrahamu akasema: “Ninaapa hivyo.”
-