-
1 Yohana 3:10-12Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
10 Watoto wa Mungu na watoto wa Ibilisi ni wazi kwa jambo hili: Yeyote ambaye haendelei kufanya uadilifu hatokani na Mungu, wala yule ambaye hampendi ndugu yake.+ 11 Kwa maana huu ndio ujumbe ambao mmesikia tangu mwanzo, kwamba tunapaswa kupendana;+ 12 si kama Kaini, aliyetokana na yule mwovu akamuua ndugu yake. Na kwa nini alimuua?+ Kwa sababu matendo yake mwenyewe yalikuwa maovu,+ lakini matendo ya ndugu yake yalikuwa ya uadilifu.+
-