-
Kutoka 25:10-15Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
10 “Mtanitengenezea sanduku la mbao za mshita lenye urefu wa mikono miwili na nusu* na upana wa mkono mmoja na nusu na kimo cha mkono mmoja na nusu.+ 11 Kisha utalifunika kwa dhahabu safi.+ Utalifunika ndani na nje na kutengeneza ukingo wa dhahabu kulizunguka.+ 12 Nawe utatengeneza pete nne za dhahabu na kuzifunga sehemu ya juu ya miguu yake minne, pete mbili upande mmoja na pete mbili upande wa pili. 13 Nawe utatengeneza fito za mshita na kuzifunika kwa dhahabu.+ 14 Utazitia fito hizo katika zile pete zilizo kwenye pande mbili za Sanduku ili zitumiwe kulibeba. 15 Fito hizo zitakaa kwenye pete za Sanduku; hazipaswi kuondolewa.+
-