-
Kutoka 38:9-11Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
9 Kisha akatengeneza ua.+ Upande wa kusini wa ua huo, alitengeneza mapazia yanayoning’inia ya kitani bora kilichosokotwa yenye urefu wa mikono 100.+ 10 Ulikuwa na nguzo 20 na vikalio 20 vya shaba, na kulabu za nguzo hizo na vitanzi* vyake vilikuwa vya fedha. 11 Pia, kulikuwa na mapazia yanayoning’inia upande wa kaskazini yenye urefu wa mikono 100. Nguzo zake 20 na vikalio vyake 20 vilikuwa vya shaba. Lakini kulabu za nguzo hizo na vitanzi* vyake vilikuwa vya fedha.
-