-
Kutoka 27:9-15Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
9 “Utatengeneza ua wa hema+ la ibada. Upande wa kusini, ua huo utakuwa na mapazia yanayoning’inia ya kitani bora kilichosokotwa; yatakuwa na urefu wa mikono 100 upande mmoja.+ 10 Ua huo utakuwa na nguzo 20 na vikalio 20 vya shaba. Kulabu za nguzo hizo pamoja na vitanzi* vyake vitakuwa vya fedha. 11 Mapazia yanayoning’inia upande wa kaskazini yatakuwa pia na urefu wa mikono 100, pamoja na nguzo zake 20 na vikalio vyake 20 vya shaba, lakini kulabu za nguzo hizo na vitanzi* vyake vitakuwa vya fedha. 12 Upande wa magharibi wa ua utakuwa na mapazia yanayoning’inia yenye urefu wa mikono 50, na nguzo 10 na vikalio 10. 13 Ua utakuwa na upana wa mikono 50 upande wa mashariki, yaani, upande wa mapambazuko ya jua. 14 Mapazia yanayoning’inia yenye upana wa mikono 15 yatakuwa upande mmoja, pamoja na nguzo tatu na vikalio vitatu.+ 15 Upande wa pili utakuwa na mapazia yanayoning’inia yenye upana wa mikono 15, pamoja na nguzo tatu na vikalio vitatu.
-