-
Kutoka 38:9-15Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
9 Kisha akatengeneza ua.+ Upande wa kusini wa ua huo, alitengeneza mapazia yanayoning’inia ya kitani bora kilichosokotwa yenye urefu wa mikono 100.+ 10 Ulikuwa na nguzo 20 na vikalio 20 vya shaba, na kulabu za nguzo hizo na vitanzi* vyake vilikuwa vya fedha. 11 Pia, kulikuwa na mapazia yanayoning’inia upande wa kaskazini yenye urefu wa mikono 100. Nguzo zake 20 na vikalio vyake 20 vilikuwa vya shaba. Lakini kulabu za nguzo hizo na vitanzi* vyake vilikuwa vya fedha. 12 Hata hivyo, upande wa magharibi ulikuwa na mapazia yanayoning’inia yenye urefu wa mikono 50. Pia ulikuwa na nguzo kumi na vikalio kumi, kulabu na vitanzi* vyake vilikuwa vya fedha. 13 Ua huo ulikuwa na upana wa mikono 50 upande wa mashariki, yaani, upande wa mapambazuko ya jua. 14 Upande mmoja ulikuwa na mapazia yanayoning’inia yenye upana wa mikono 15, pamoja na nguzo tatu na vikalio vitatu. 15 Upande wa pili wa mlango wa ua ulikuwa na mapazia yanayoning’inia yenye upana wa mikono 15, pamoja na nguzo tatu na vikalio vyake vitatu.
-