-
Kutoka 10:16-19Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
16 Basi Farao akawaita haraka Musa na Haruni na kuwaambia: “Nimemtendea dhambi Yehova Mungu wenu na ninyi pia. 17 Sasa, tafadhali, mnisamehe dhambi yangu mara hii moja tu, na kumsihi Yehova Mungu wenu angalau aniondolee pigo hili hatari.” 18 Basi akaondoka* kwa Farao na kumsihi Yehova.+ 19 Kisha Yehova akasababisha upepo huo ubadili mkondo, nao ukawa upepo wenye nguvu sana wa magharibi, ukawapeperusha nzige hao na kuwapeleka katika Bahari Nyekundu. Hakuna nzige hata mmoja aliyebaki katika eneo lote la Misri.
-