-
Kumbukumbu la Torati 6:20-22Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
20 “Wakati ujao, mwana wako akikuuliza, ‘Vikumbusho, masharti, na sheria* ambazo Yehova Mungu wetu ametuamuru tushike zinamaanisha nini?’ 21 ndipo utakapomwambia mwana wako, ‘Tulikuwa watumwa wa Farao kule Misri, lakini Yehova alitutoa Misri kwa mkono wenye nguvu. 22 Basi mbele ya macho yetu, Yehova aliendelea kufanya ishara na miujiza mikubwa na iliyoleta uharibifu nchini Misri,+ na pia kwa Farao na nyumba yake yote.+
-