-
Matendo 7:30-34Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
30 “Baada ya miaka 40, malaika akamtokea kwenye nyika ya Mlima Sinai katika mwali wa moto wa kichaka cha miiba kilichokuwa kikiwaka.+ 31 Musa alipoona jambo hilo, akashangaa sana. Lakini alipokaribia ili kuchunguza, akasikia sauti ya Yehova* ikisema: 32 ‘Mimi ni Mungu wa mababu zako, Mungu wa Abrahamu na wa Isaka na wa Yakobo.’+ Musa akaanza kutetemeka na hakuthubutu kuchunguza zaidi. 33 Yehova* akamwambia, ‘Vua viatu vyako, kwa maana mahali unaposimama ni ardhi takatifu. 34 Hakika nimeona jinsi watu wangu walio Misri wanavyokandamizwa, nimesikia kilio chao cha huzuni,+ nami nimeshuka ili kuwaokoa. Basi njoo, nitakutuma huko Misri.’
-