-
Kutoka 5:19Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
19 Kwa hiyo wasimamizi wa Waisraeli wakatambua kwamba wako katika shida kubwa kwa sababu ya amri hii: “Msipunguze hata kidogo idadi ya matofali mnayopaswa kufyatua kila siku.”
-
-
Hesabu 14:2, 3Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
2 Waisraeli wote wakaanza kumnung’unikia Musa na Haruni,+ na wote wakawalalamikia wakisema: “Laiti tungalifia katika nchi ya Misri, au laiti tungalifia hapa nyikani! 3 Kwa nini Yehova anatuleta kwenye nchi hii ili tuuawe kwa upanga?+ Wake zetu na watoto wetu watakuwa mateka.+ Je, si afadhali turudi Misri?”+
-