-
Waebrania 12:18-21Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
18 Kwa maana hamkukaribia kitu kinachoweza kuguswa+ na ambacho kimewashwa moto,+ na wingu jeusi na giza zito na dhoruba,+ 19 na mlio wa tarumbeta+ na sauti ya maneno yanayosemwa,+ ambayo watu walipoisikia waliomba kwamba wasiambiwe neno lingine lolote.+ 20 Kwa maana hawakuweza kuivumilia amri hii: “Hata mnyama akiugusa mlima, lazima apigwe mawe.”+ 21 Pia, wonyesho huo ulikuwa wa kutisha sana hivi kwamba Musa akasema: “Ninaogopa na kutetemeka.”+
-