-
Kutoka 24:17Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
17 Kwa Waisraeli waliokuwa wakitazama, utukufu wa Yehova ulionekana kama moto mkali kwenye kilele cha mlima.
-
-
2 Mambo ya Nyakati 7:1-3Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
7 Basi, mara tu Sulemani alipomaliza kusali,+ moto ulishuka kutoka mbinguni+ ukateketeza ile dhabihu ya kuteketezwa na dhabihu nyinginezo, na utukufu wa Yehova ukajaa katika nyumba hiyo.+ 2 Makuhani hawakuweza kuingia ndani ya nyumba ya Yehova kwa sababu utukufu wa Yehova ulikuwa umejaa katika nyumba ya Yehova.+ 3 Waisraeli wote walikuwa wakitazama moto uliposhuka na utukufu wa Yehova ulipokuwa juu ya nyumba hiyo, nao wakainama kifudifudi kwenye sakafu ya mawe, wakasujudu na kumshukuru Yehova, “kwa maana yeye ni mwema; upendo wake mshikamanifu unadumu milele.”
-