-
Kutoka 37:17-24Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
17 Halafu akatengeneza kinara cha taa kwa dhahabu safi.+ Alikitengeneza kinara hicho cha taa kwa nyundo. Sehemu yake ya chini, shina lake, matawi yake, vikombe vyake, matumba yake, na maua yake yalitengenezwa kwa kipande kimoja cha dhahabu.+ 18 Kinara hicho kilikuwa na matawi sita, matawi matatu upande mmoja na matawi matatu upande wa pili. 19 Kila tawi lilikuwa na vikombe vitatu vyenye umbo la maua ya mlozi, na kila kikombe kilikuwa na ua na tumba lake. Hivyo ndivyo matawi hayo sita yalivyotengenezwa kwenye shina la kinara hicho cha taa. 20 Shina la kinara lilikuwa na vikombe vinne vyenye umbo la maua ya mlozi, kila kikombe kilikuwa na ua na tumba lake. 21 Kulikuwa na tumba chini ya jozi ya kwanza ya matawi hayo sita, tumba chini ya jozi ya pili, na tumba chini ya jozi ya tatu. 22 Matumba na matawi yake na kinara chote cha taa kilitengenezwa kwa kipande kimoja cha dhahabu safi, kwa kutumia nyundo. 23 Kisha akatengeneza taa saba+ pamoja na koleo zake na vyetezo vyake kwa dhahabu safi. 24 Alitumia talanta moja* ya dhahabu safi kutengeneza kinara hicho na vifaa vyake vyote.
-