-
Kutoka 29:1-3Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
29 “Hivi ndivyo utakavyowatakasa ili wanitumikie wakiwa makuhani: Chukua ng’ombe dume mchanga, kondoo dume wawili wasio na kasoro,+ 2 mikate isiyo na chachu, mikate ya mviringo isiyo na chachu na iliyokandwa kwa mafuta, na mikate myembamba isiyo na chachu na ambayo imepakwa mafuta.+ Utaioka kwa unga laini wa ngano 3 na kuiweka ndani ya kikapu, nawe utaileta mbele zangu ikiwa ndani ya kikapu,+ pamoja na yule ng’ombe dume na wale kondoo dume wawili.
-
-
Mambo ya Walawi 6:14, 15Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
14 “‘Hii ndiyo sheria kuhusu toleo la nafaka:+ Ninyi wana wa Haruni mtamtolea Yehova toleo hilo mbele ya madhabahu. 15 Mmoja wenu atachukua mkono mmoja wa unga laini wa toleo la nafaka na kiasi fulani cha mafuta yake na ubani wote ulio katika toleo la nafaka, naye atauteketeza ili ufuke moshi kwenye madhabahu kama harufu ya kupendeza* ya dhabihu ya kumbukumbu* kwa Yehova.+
-