-
Kutoka 29:15-18Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
15 “Kisha utamchukua kondoo dume mmoja, naye Haruni na wanawe wataweka mikono yao juu ya kichwa cha huyo kondoo dume.+ 16 Mchinje kondoo dume huyo, uchukue damu yake na kuinyunyiza pande zote za madhabahu.+ 17 Mkate kondoo dume huyo vipandevipande, uoshe matumbo yake+ na miguu yake, na kuvipanga vipande hivyo pamoja na kichwa chake. 18 Utamchoma moto huyo kondoo mzima ili afuke moshi juu ya madhabahu. Ni dhabihu ya kuteketezwa kwa Yehova, harufu inayompendeza.*+ Ni dhabihu kwa Yehova inayochomwa kwa moto.
-
-
Mambo ya Walawi 1:4Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
4 Ataweka mkono wake juu ya kichwa cha dhabihu hiyo ya kuteketezwa, nayo itakubaliwa kwa niaba yake ili kufunika dhambi zake.
-