-
Mambo ya Walawi 5:11, 12Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
11 “‘Ikiwa hawezi kutoa njiwa tetere wawili au hua wawili wachanga, basi atatoa sehemu ya kumi ya kipimo cha efa moja*+ ya unga laini ili kuwa dhabihu ya dhambi. Hapaswi kuutia mafuta au ubani kwa sababu ni dhabihu ya dhambi. 12 Atauleta kwa kuhani, naye kuhani atachukua mkono mmoja wa unga huo ukiwa dhabihu ya kumbukumbu* naye atauweka kwenye madhabahu juu ya dhabihu za Yehova zinazochomwa kwa moto ili ufuke moshi. Ni dhabihu ya dhambi.
-
-
Mambo ya Walawi 6:14, 15Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
14 “‘Hii ndiyo sheria kuhusu toleo la nafaka:+ Ninyi wana wa Haruni mtamtolea Yehova toleo hilo mbele ya madhabahu. 15 Mmoja wenu atachukua mkono mmoja wa unga laini wa toleo la nafaka na kiasi fulani cha mafuta yake na ubani wote ulio katika toleo la nafaka, naye atauteketeza ili ufuke moshi kwenye madhabahu kama harufu ya kupendeza* ya dhabihu ya kumbukumbu* kwa Yehova.+
-