-
Mambo ya Walawi 7:23-25Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
23 “Waambie Waisraeli, ‘Hampaswi kula mafuta yoyote+ ya ng’ombe dume au ya mwanakondoo dume au ya mbuzi. 24 Mafuta ya mnyama aliyepatikana amekufa na mafuta ya mnyama aliyeuawa na mnyama mwingine, yanaweza kutumiwa kwa kusudi lingine lolote, lakini hampaswi kamwe kuyala.+ 25 Kwa maana mtu yeyote anayekula mafuta ya mnyama anayemtoa kuwa dhabihu kwa Yehova inayochomwa kwa moto, ni lazima auawe.
-
-
1 Wafalme 8:64Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
64 Siku hiyo ilimbidi mfalme atakase sehemu ya katikati ya ua ulio mbele ya nyumba ya Yehova, kwa sababu alipaswa kutolea mahali hapo dhabihu za kuteketezwa, matoleo ya nafaka, na vipande vya mafuta vya dhabihu za ushirika, kwa sababu madhabahu ya shaba+ iliyo mbele za Yehova ilikuwa ndogo sana isiweze kutoshea dhabihu za kuteketezwa, matoleo ya nafaka, na vipande vya mafuta+ vya dhabihu za ushirika.
-