-
Mambo ya Walawi 25:25-27Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
25 “‘Ikiwa ndugu yako atakuwa maskini na hivyo alazimike kuuza sehemu fulani ya urithi wake, basi mkombozi ambaye ni mtu wake wa karibu wa ukoo atakuja na kununua sehemu iliyouzwa na ndugu yake.+ 26 Ikiwa mtu hana mkombozi lakini anapata ufanisi na kupata uwezo wa kuikomboa, 27 anapaswa kuhesabu thamani yake kulingana na miaka iliyopita tangu alipoiuza na kumrudishia yule aliyeinunua kiasi kinachobaki. Kisha atarudi kwenye urithi wake.+
-