-
Ruthu 4:4-6Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
4 Niliona nikufahamishe jambo hilo na kukwambia, ‘Linunue mbele ya wakaaji na wazee wa watu wangu.+ Ikiwa utalikomboa, likomboe. Lakini ikiwa hutalikomboa, niambie ili nijue, kwa maana una haki ya kulikomboa, mimi ni wa pili.’” Mtu huyo akasema: “Niko tayari kulikomboa.”+ 5 Kisha Boazi akamwambia: “Siku utakapolinunua shamba hilo kutoka kwa Naomi, unapaswa kulinunua pia kutoka kwa Ruthu Mmoabu, mke wa mwanamume aliyekufa, ili kurudisha jina la mume wake aliyekufa katika urithi huo.”+ 6 Basi mkombozi huyo akasema: “Siwezi kulikomboa kwa maana huenda nikaharibu urithi wangu mwenyewe. Likomboe kwa ajili yako mwenyewe ukitumia haki yangu ya kukomboa, kwa sababu siwezi kulikomboa.”
-