-
Mambo ya Walawi 27:11-13Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
11 Ikiwa ni mnyama asiye safi+ ambaye hawezi kutolewa kwa Yehova, mnyama huyo atapelekwa mbele ya kuhani. 12 Halafu kuhani atakadiria thamani yake, ataamua ikiwa ni mzuri au mbaya. Thamani itakayokadiriwa na kuhani ndiyo itakayokuwa thamani ya mnyama huyo. 13 Lakini ikiwa mtu huyo anataka kumnunua tena mnyama huyo, ni lazima alipe thamani ya mnyama huyo pamoja na sehemu ya tano ya thamani iliyokadiriwa.+
-