36 Kwa siku saba mtamtolea Yehova dhabihu inayochomwa kwa moto. Siku ya nane mtakuwa na kusanyiko takatifu,+ nanyi mnapaswa kumtolea Yehova dhabihu inayochomwa kwa moto. Ni kusanyiko takatifu. Hampaswi kufanya kazi yoyote ngumu.
39 Hata hivyo, siku ya 15 ya mwezi wa saba, baada ya kukusanya mavuno yenu, mnapaswa kufanya sherehe ya Yehova kwa siku saba.+ Siku ya kwanza ni ya pumziko kamili na siku ya nane ni ya pumziko kamili.+