132 Ee Yehova, mkumbuke Daudi
Na mateso yake yote;+
2 Jinsi alivyomwapia Yehova,
Jinsi alivyomwekea nadhiri hii Mwenye Nguvu wa Yakobo:+
3 “Sitaingia katika hema langu, nyumbani mwangu.+
Sitalala kwenye kochi langu, kitandani mwangu;
4 Sitayaruhusu macho yangu yalale usingizi,
Wala kope zangu kusinzia
5 Mpaka nitakapopata mahali kwa ajili ya Yehova,
Makao bora kwa ajili ya Mwenye Nguvu wa Yakobo.”+