-
Hesabu 3:25, 26Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
25 Majukumu ya wana wa Gershoni+ katika hema la mkutano yalikuwa kutunza hema lenyewe pamoja+ na kifuniko chake,+ pazia+ la mlango wa hema la mkutano, 26 mapazia ya ua yanayoning’inia,+ pazia la mlango wa ua+ linalozunguka hema la ibada na madhabahu, kamba za hema, na utumishi wote uliohusiana na vitu hivyo.
-
-
Hesabu 4:24-26Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
24 Huu ndio utumishi ambao watu wa familia za Wagershoni wamegawiwa kufanya na vitu wanavyopaswa kubeba:+ 25 Watabeba vitambaa vya hema la ibada,+ hema la mkutano, kifuniko chake na kifuniko cha ngozi ya sili kilicho juu yake,+ pazia la mlango wa hema la mkutano,+ 26 mapazia ya ua yanayoning’inia,+ pazia la mlango wa ua+ unaozunguka hema la ibada na madhabahu, kamba za hema hilo na vyombo vyake vyote, na vitu vyote vinavyotumiwa katika utumishi wa hema la ibada. Hiyo ndiyo kazi waliyogawiwa.
-