-
Mwanzo 48:17-19Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
17 Yosefu hakufurahi alipoona baba yake ameuweka mkono wake wa kulia juu ya kichwa cha Efraimu, basi akashika mkono wa baba yake na kujaribu kuuondoa juu ya kichwa cha Efraimu ili auweke juu ya kichwa cha Manase. 18 Yosefu akamwambia baba yake: “Sivyo baba yangu, kwa kuwa huyu ndiye mzaliwa wa kwanza.+ Weka mkono wako wa kulia juu ya kichwa chake.” 19 Lakini baba yake akazidi kukataa na kusema: “Najua, mwanangu, najua. Yeye pia atakuwa taifa, yeye pia atakuwa mkuu. Hata hivyo, ndugu yake mdogo atakuwa mkuu kuliko yeye,+ na uzao wake utalingana* kabisa na mataifa.”+
-