Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mwanzo 41:51, 52
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 51 Yosefu alimwita mzaliwa wa kwanza Manase,*+ kwa maana alisema, “Mungu amenifanya nisahau taabu yangu yote na nyumba yote ya baba yangu.” 52 Akamwita yule wa pili Efraimu,*+ kwa maana alisema, “Mungu ameniwezesha kuzaa watoto katika nchi ya mateso yangu.”+

  • Mwanzo 46:20
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 20 Katika nchi ya Misri, Asenathi+ binti ya Potifera kuhani wa Oni,* alimzalia Yosefu wana hawa: Manase+ na Efraimu.+

  • Mwanzo 48:17-19
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 17 Yosefu hakufurahi alipoona baba yake ameuweka mkono wake wa kulia juu ya kichwa cha Efraimu, basi akashika mkono wa baba yake na kujaribu kuuondoa juu ya kichwa cha Efraimu ili auweke juu ya kichwa cha Manase. 18 Yosefu akamwambia baba yake: “Sivyo baba yangu, kwa kuwa huyu ndiye mzaliwa wa kwanza.+ Weka mkono wako wa kulia juu ya kichwa chake.” 19 Lakini baba yake akazidi kukataa na kusema: “Najua, mwanangu, najua. Yeye pia atakuwa taifa, yeye pia atakuwa mkuu. Hata hivyo, ndugu yake mdogo atakuwa mkuu kuliko yeye,+ na uzao wake utalingana* kabisa na mataifa.”+

  • Hesabu 2:18, 19
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 18 “Kundi la makabila matatu katika kambi ya Efraimu litapiga kambi upande wa magharibi, kulingana na vikosi vyake;* mkuu wa wana wa Efraimu ni Elishama+ mwana wa Amihudi. 19 Wale walioandikishwa katika jeshi lake ni watu 40,500.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki