19 Kwa siku saba, unga uliokandwa ambao umetiwa chachu usipatikane ndani ya nyumba zenu, kwa sababu yeyote akila kitu kilichotiwa chachu, awe ni mgeni au mwenyeji wa nchi,+ mtu huyo lazima auawe kutoka katika kusanyiko la Israeli.+
48 Ikiwa mgeni anaishi pamoja nawe, naye anataka kusherehekea Pasaka ya Yehova, ni lazima kila mwanamume wa familia yake atahiriwe. Kisha anaweza kukaribia ili kuisherehekea, naye atakuwa kama mwenyeji wa nchi. Lakini mwanamume yeyote ambaye hajatahiriwa hapaswi kuila Pasaka.+