26 “‘Hata hivyo, hakuna mtu yeyote anayepaswa kumtakasa mzaliwa wa kwanza wa wanyama, kwa sababu mzaliwa wa kwanza ni wa Yehova.+ Awe ni ng’ombe dume au kondoo, tayari ni wa Yehova.+
13 Kwa maana kila mzaliwa wa kwanza ni wangu.+ Siku niliyomuua kila mzaliwa wa kwanza katika nchi ya Misri+ nilijitakasia kila mzaliwa wa kwanza katika Israeli kuanzia mzaliwa wa kwanza wa mwanadamu mpaka wa mnyama.+ Watakuwa wangu. Mimi ni Yehova.”