-
Yoshua 12:4-6Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
4 Pia, eneo la Mfalme Ogu+ wa Bashani, aliyekuwa kati ya Warefaimu+ waliosalia, ambaye aliishi Ashtarothi na Edrei 5 na kutawala katika eneo la Mlima Hermoni, Saleka, na Bashani yote,+ hadi mpaka wa Wageshuri na Wamaakathi,+ na nusu ya Gileadi, hadi katika eneo la Mfalme Sihoni wa Heshboni.+
6 Musa mtumishi wa Yehova pamoja na Waisraeli waliwashinda,+ kisha Musa mtumishi wa Yehova akawapa nchi hiyo watu wa kabila la Rubeni, Gadi, na nusu ya kabila la Manase ili waimiliki.+
-