7 Walipigana na Wamidiani, kama Yehova alivyomwamuru Musa, wakawaua wanaume wote. 8 Miongoni mwa watu waliouawa kulikuwepo wafalme watano wa Midiani, yaani, Evi, Rekemu, Suri, Huru, na Reba. Pia, walimuua kwa upanga Balaamu+ mwana wa Beori.
21 majiji yote kwenye uwanda wa juu, na eneo lote la Mfalme Sihoni wa Waamori, aliyetawala Heshboni.+ Musa alimshinda yeye+ pamoja na wakuu wa Midiani, yaani, Evi, Rekemu, Suri, Huru, na Reba,+ watawala vibaraka* wa Sihoni waliokaa nchini humo.