8 Nitashuka huko ili niwaokoe kutoka mikononi mwa Wamisri+ na kuwapandisha kutoka katika nchi hiyo na kuwapeleka katika nchi nzuri na kubwa, nchi inayotiririka maziwa na asali,+ eneo la Wakanaani, Wahiti, Waamori, Waperizi, Wahivi, na Wayebusi.+
7 Geukeni na kuelekea katika eneo lenye milima la Waamori+ na kwa majirani wao wote kule Araba,+ katika eneo lenye milima, Shefela, Negebu, pwani ya bahari,+ nchi ya Wakanaani, na Lebanoni,*+ hadi kwenye ule mto mkubwa, Mto Efrati.+
11 Lakini nchi mnayokaribia kuvuka kuingia humo ili kuimiliki ni nchi yenye milima na mabonde tambarare.+ Inanyweshwa na maji ya mvua kutoka mbinguni;+12 ni nchi inayotunzwa na Yehova Mungu wenu. Macho ya Yehova Mungu wenu yanaitazama daima, kuanzia mwanzo wa mwaka mpaka mwisho wa mwaka.