-
Mambo ya Walawi 11:13-20Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
13 “‘Hawa ndio ndege mnaopaswa kuchukia; wasiliwe kwa sababu ni chukizo: tai,+ furukombe, tumbusi* mweusi,+ 14 mwewe mwekundu na aina zote za mwewe weusi, 15 kila aina ya kunguru, 16 mbuni, bundi, shakwe, kila aina ya kipanga, 17 bundi mdogo, mnandi, bundi mwenye masikio marefu, 18 batamaji, mwari, tumbusi,* 19 korongo, kila aina ya kulastara, hudihudi, na popo. 20 Kila kiumbe mwenye mabawa* anayeishi katika makundi makubwa anayetambaa kwa miguu yote minne ni chukizo kwenu.
-