36 Kwa siku saba mtamtolea Yehova dhabihu inayochomwa kwa moto. Siku ya nane mtakuwa na kusanyiko takatifu,+ nanyi mnapaswa kumtolea Yehova dhabihu inayochomwa kwa moto. Ni kusanyiko takatifu. Hampaswi kufanya kazi yoyote ngumu.
40 Siku ya kwanza, mtachukua matunda ya miti yenu bora, matawi ya mitende,+ matawi ya miti yenye majani mengi na mierebi ya bondeni, nanyi mtashangilia+ mbele za Yehova Mungu wenu kwa siku saba.+
18 Na siku baada ya siku kitabu cha Sheria ya Mungu wa kweli kilikuwa kikisomwa,+ tangu siku ya kwanza hadi siku ya mwisho. Nao wakafanya sherehe hiyo kwa siku saba, na siku ya nane walifanya kusanyiko takatifu, kama ilivyoagizwa.+