-
Kumbukumbu la Torati 21:6-9Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
6 Kisha wazee wote wa jiji lililo karibu zaidi na maiti hiyo wanapaswa kunawa mikono yao+ juu ya ng’ombe huyo mchanga ambaye alivunjwa shingo bondeni, 7 nao wanapaswa kutangaza hivi: ‘Mikono yetu haikumwaga damu hii, wala macho yetu hayakuona ikimwagwa. 8 Usiwahesabie hatia hiyo watu wako Waisraeli, ambao uliwakomboa,+ Ee Yehova, nawe usiache hatia ya damu isiyo na lawama ibaki miongoni mwa watu wako Waisraeli.’+ Nao hawatakuwa na hatia hiyo ya damu. 9 Kwa njia hiyo mtaondoa hatia ya damu isiyo na lawama kutoka miongoni mwenu kwa kufanya yaliyo sawa machoni pa Yehova.
-